• Malalamiko |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Wafanyakazi |
Biharamulo District Council Website
Biharamulo District Council Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Misingi
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Miundombinu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uasfi na Mazingira
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Furusa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
    • Kamati za Kudumu
  • Miradi
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mapato na Matumizi Robo ya Tatu
    • Jarida la eGA Toleo 6 na 9
    • Bajeti ya Mwaka 2023-2024
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Mkutano wa Baraza la Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Ofisi

TATHMINI YA MAAFA YA MVUA YA UPEPO ILIYONYESHA KATA ZA BIHARAMULO

07 December 2017

Tarehe 29/11/2017 majira ya saa sita mchana, mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali na mawe ilinyesha katika Kata tajwa hapo juu na kusababisha nyumba kadhaa kuezuliwa na mazao mashambani kuharibiwa.

Aidha hakukutokea majeruhi wala vifo vilivyotokana na maafa kwenye maeneo hayo.

MADHARA YALIYOTOKEA KWENYE MAAFA HAYO

  1. Kata ya Biharamulo mjini

Jumla ya nyumba 14 ziliharibiwa katika viwango mbalimbali, hasa kuezuliwa kwa mapaa.

Hakuna vifo wala majeruhi na angalau waathirika wote wana mahali wanapojihifadhi katika vyumba ambavyo havijaathirika katika maeneo yao na waathirika wao wenyewe na kwa kusaidiwa na majirani wanafanya jitihada za kuezeka mapaa yaliyoezuliwa.

  1. Kata ya Runazi

Jumla ya nyumba 34 katika kijiji cha Ruziba, Kata ya Ruziba yenye vijiji 4 na kijiji pekee kilichoathiriwa na maafa hayo katika Kata hiyo. Kijiji hicho chenye Jumla ya kaya 560 pia kimeathirika kati kilimo ,kwani jumla ya ekari 142.5 zimeharibiw katika viwango tofauti. Athari katika mazao ni kama ifuatavyo:-

Migomba ekari 56

Mahindi ekari   54

Maharage ekari 29

Mazao ya bustani ekari 2.5

Jumla ni ekari 142.5.

TATHMINI  YA AWALI ILIYOFANYWA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA NA KAMATI YA MAAFA YA WILAYA

Baada ya Kamati tajwa hapo juu kushuhudia maafa hayo katika maeneo yaliyoathiriwa ilibaini mambo yafuatayo kama ndio yaliyochochea maafa hayo kuwa makubwa:-

Nyumba nyingi zilizoezuliwa ni zile zilizochakaa (zenye umri mkubwa) na na ambazo hazikuezekwa kwa mujibu wa taratibu za kiufundi.

Hakuna majeruhi wala vifo vilivyotokea katika maafa haya.

Nyumba za taasisi zilizoezuliwa ni jingo la Jeshi la Akiba (Mgambo) mjini Biharamulo.

Mazao yameharibiwa na mawe na upepo mkali mfano migomba, mahindi, maharage na mazao ya bustani. Aidha zao la mahindi halitaathirika sana kwani tunatarajia yatakua vizuri kwani mengi yako katika hatua za awali z ukuaji. Maharage na mazao ya bustani yameharibika kwa kiwango cha wastani. Migomba mingi iliyoharibika haitovunwa hadi vichipukizi vitakapokuwa ingawa haiwezi kusababisha uksefu wa chakula kwa waathirika.

MAELEKEZO NA USHAURI WA KAMATI

Wananchi washauriwe kufanya ujenzi wa nyumba kwa kufuata utaalamu ili kuepuka kutokea kwa ajali zisizokuwa za lazima.

Majirani, ndugu jamaa na marafiki wawasaidie waathirika kuweza kuezeka upya nyumba zao na kuwasaidia sehemu za kulala wakati wakipaua nyumba zao.

Halmashauri ya wilaya ifanye jitihada haraka za kupaua nyumba ya mwalimu iliyoezuliwa ili mwalimu aendelee kuishi maeneo ya shule.

Nyumba ya Jeshi la Mgambo itakarabatiwa na wahusika na kwa muda wahamishie shughuli zao  kwenye majengo mengine waliyoyajenga.

Wananchi washauriwe kupanda miti kwenye makazi yao ili kukinga upepo usiezue nyumba zao, kwani nyumb zote zilizokwenye miti katika maeneo yaliyoathirika hazikuezuliwa.

Katika maafa haya hakuna muathirika ambaye maafa haya yamesababisha upungufu/ukosefu wa chakula kwa sasa.

    

Cornel P. Mwasote

Mratibu wa Maafa (w),

BIHARAMULO.

Matangazo

  • TANGAZO KUHUSU UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA August 30, 2024
  • TANGAZO LA KUSHIRIKI UCHACUZI WA SERIKALI ZA MITAA November 23, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHAJI VIFAA BAYOMETRIKI July 18, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • Mkurugenzi wa Uchaguzi Ndugu Ramadhani Kailima amewataka Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Tanzania bara kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

    June 16, 2024
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI SEHEMU YA PILI YA MPANGO HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO

    January 03, 2024
  • Waajiriwa wapya Division ya Afya na Elimu Juni, 2023

    June 07, 2023
  • MKUU WA MKOA WA KAGERA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI BIHARAMULO

    November 30, 2022
  • Tazama zaidi

Video

MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWAKA 2022 WILAYANI BIHARAMULO
Video Zaidi

Kuarasa za Haraka

  • Historia

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Tovuti ya Manispaa ya Bukoba
  • Tovuti ya wilaya ya Muleba
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Kuwasiliana nasi

    Mtaa wa Bomani

    Sanduku la Barua: S.L.P 70

    Telephone: 028 2223403

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@biharamulodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya Biharamulo. Haki zote zimehifadhiwa