• Malalamiko |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Wafanyakazi |
Biharamulo District Council Website
Biharamulo District Council Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Misingi
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Miundombinu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uasfi na Mazingira
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Furusa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
    • Kamati za Kudumu
  • Miradi
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mapato na Matumizi Robo ya Tatu
    • Jarida la eGA Toleo 6 na 9
    • Bajeti ya Mwaka 2023-2024
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Mkutano wa Baraza la Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Ofisi

MKUU WA MKOA WA KAGERA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI BIHARAMULO

Posted on: November 30th, 2022

Mhe. Albert John Chalamila ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera, amefanya ziara na kukagua Miradi ya Maendeleo ili kujiridhisha na hali halisi iliyopo.

Miongoni mwa wataalam alioambatana nao katika ziara hiyo iliyoendelea katika Kata za Biharamulo Mjini, Kabindi, Nyamigogo, Nyakanazi na Nyakahura ni Katibu Tawala Msaidizi(M) upande wa Miundombinu, Afisa Habari na Mawasiliano Serikalini wa Mkoa na Afisa  Utumishi na Utawala wa Mkoa.

Wengine alioambatana nao ni pamoja na Kaimu Katibu Tawala (W), Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Diwani Kata ya Nyantakara, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Wakuu wa Divisheni na Vitengo wa Halmashauri, Kaimu Afisa Tarafa ya Nyarubungo na Wakuu wa Taasisi za Umma.

Kiongozi huyo amekagua miradi wa ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya katika Kata ya Biharamulo Mjini, mradi wa ujenzi wa vyumba tisa (9) vya madarasa Shule ya Sekondari Runazi iliyopo Kata ya Kabindi, Kijiji cha Kikomakoma.

Miradi mingine iliyotembelewa na Mhe. Chalamila ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Vyumba kumi na saba (17) vya madarasa katika Shule ya Sekondari Nyakanazi iliyopo Kata ya Lusahunga, Kijiji cha Nyakanazi na Mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari iliyopo Kata ya Nyakahura, Kijiji cha Ngararambe.

Wakati huo huo Mhe. Chalamila ametembelea walengwa (38) walioguswa na Mradi wa Bomba la Mafuta na kuongea na Wananchi kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa mpira wa Shule ya Msingi Kasozibakaya Kata ya Nyamigogo.

Chalamila amepongeza wasimamizi wote wa miradi yote aliyotembelea na kuagiza wataalam wa Mkoa watembelee miradi yote hasa yenye madarasa mengi mfano Nyakanazi na Runazi Sekondari zenye madarasa 17 na 9 na kutoa ushauri wa kitaalam inapo bidi kufanya hivyo.

“Mhandisi tembeleeni haraka hizi Shule zenye miradi mikubwa kama hii Shule ya Nyakanazi imepokea Tshs. 340,000,000 kwa ajili ya kujenga vyumba vya madarasa 17 ili mtoe ushauri wa kitaalam pale inapobidi kufanya hivyo ”

Ameyasema hayo leo tarehe 30 Novemba 2022 akiwa katika ziara yake ya kikazi Wilayani Biharamulo siku ambayo ameitumia kuwakumbusha wafanyakazi wa Halmashauri kuhudumia wananchi, Walimu wajitahidi kupunguza divisheni 4 na zero na Wanafunzi wasome kwa bidii ili baadaye washike nyadhifa mbalimbali kama Wakuu wa Mikoa, Wilaya na kada mbalimbali. Amewasistiza wanafunzi wasifanya zinaa kwa kuwa ni chanzo cha mimba za utotoni, magonjwa ya zinaa pamoja na ugonjwa wa Ukimwi.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO May 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHAJI VIFAA BAYOMETRIKI July 18, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • Tangazo la utoaji wa Mikopo ya Halmasahauri October 08, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • Mkurugenzi wa Uchaguzi Ndugu Ramadhani Kailima amewataka Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Tanzania bara kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

    June 16, 2024
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI SEHEMU YA PILI YA MPANGO HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO

    January 03, 2024
  • Waajiriwa wapya Division ya Afya na Elimu Juni, 2023

    June 07, 2023
  • MKUU WA MKOA WA KAGERA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI BIHARAMULO

    November 30, 2022
  • Tazama zaidi

Video

MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWAKA 2022 WILAYANI BIHARAMULO
Video Zaidi

Kuarasa za Haraka

  • Historia

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Tovuti ya Manispaa ya Bukoba
  • Tovuti ya wilaya ya Muleba
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Kuwasiliana nasi

    Mtaa wa Bomani

    Sanduku la Barua: S.L.P 70

    Telephone: 028 2223403

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@biharamulodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya Biharamulo. Haki zote zimehifadhiwa