• Malalamiko |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Wafanyakazi |
Biharamulo District Council Website
Biharamulo District Council Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Misingi
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Miundombinu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uasfi na Mazingira
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Furusa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
    • Kamati za Kudumu
  • Miradi
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mapato na Matumizi Robo ya Tatu
    • Jarida la eGA Toleo 6 na 9
    • Bajeti ya Mwaka 2023-2024
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Mkutano wa Baraza la Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Ofisi

Miradi ya Maendeleo itakayo tembelewa na Mwenge wa Uhuru 2019 tarehe 01/05/2019

Monday 2nd, June 2025
@Biharamulo

MRADI WA KILIMO BORA CHA MIGOMBA LENYE EKARI MBILI (2)

GHARAMA ZA MRADI

Mradi huu ulianzishwa tarehe 27/12/2017 kwa kupanda migomba ya kisasa aina ya FHIA 17 na FHIA 23 lenye jumla ya miche 888, lengo la kuanzisha kilimo hiki ni kuinua hali ya kiuchumi na familia kwa ujumla. Mpaka sasa mradi huu umeghalimu Tsh. 4,780,000/=. Gharama hizi zinajumuisha maandalizi ya shamba, uchimbaji wa mashimo, ununuzi wa samadi, ununuzi wa miche bora, palizi, ununuzi wa nyasi za kutandazia shamba pamoja na usafi wa shamba kwa ujumla.


HALI YA UZALISHAJI  WA MIKUNGU YA NDIZI

Mradi huu kwa sasa una uwezo wa kuzalisha mikungu 800 kwa mwaka, yenye uzito wa wastani wa kilo 50 kwa kila mkungu na zenye wastani wa bei ya kuuzia ya  Tsh.8000/= kwa mkungu na matarajio ya kunipatia wastani wa Tsh. 6,400,000/= kwa mwaka.

Mradi huu umekuwa chanzo cha mapato kwa familia, pia umenisaidia kutoa ajira katika jamii, zaidi ya watu 49 (Me 19 na Ke 30) wamepata ajira katika mradi huu tangu maandalizi ya shamba hadi sasa. Kazi zilizofanyika ni pamoja na uchimbaji wa mashimo, palizi, usombaji wa mbolea (samadi) na kupunguzia miche. Aidha, Wakulima 8 wamenufaika na uwepo wa shamba hili kwa kupata zaidi ya miche 1776 na kwenda kupanda kwenye mashamba yao kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo cha migomba.


Mafanikio ya mradi huu yametokana na ushauri wa Wataalamu wa Ugani katika kata hii ya Nyabusozi. Matarajio yangu ni kuongeza uzalishaji na kufikia mapato ya Tsh. 8,000,000/= kwa mwaka. Hakika kilimo hiki kitanisaidia sana kuboresha maisha yangu.


MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA MAHAKAMA YA MWANZO – STENDI - DDH KM MOJA (1)


Mradi huu umetekelezwa katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa kutumia fedha za mfuko wa Barabara, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa ahadi ya Mhe.Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 tulijenga kilometa moja (1) ya Barabara kwa kiwango cha lami ambayo leo tarehe 01/05/2019 tunaomba izinduliwe na Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Kitaifa.
Mradi huu umetekelezwa na mkandarasi M/S KAJUNA INVESTIMENT COMPANY LTD na ulianza tarehe 02/02/2018 na umekamilika tarehe 28/06/2018, kwa gharama ya Tshs. 298,186,000/= ikiwa ni pamoja na kodi ya ongezeko la Thamani (VAT.)

HALI YA UTEKELEZAJI.
Hadi sasa mradi huu umekamilika kwa hatua zote zilizoidhinishwa kwenye mkataba ambazo ni ujenzi wa tabaka la kwanza la barabara (Sub grade), tabaka la pili la ujenzi wa barabara (Sub base), ujenzi wa tabaka la tatu la barabara (Base course) pamoja na kuweka lami (Wearing course) pamoja na ujenzi wa mifereji ya mawe (stone pitch) yenye urefu wa 800m2, na  mradi huu kwa sasa upo chini ya uangalizi wa mkandarasi hadi tarehe 28/06/2019.

FAIDA ZA MRADI HUU.
Baadhi ya faida ambazo wananchi watanufaika nazo kutokana na ujenzi wa barabara ya lami ni pamoja na;-
1. Barabara itadumu kwa muda mrefu bila matengenezo ya mara kwa mara
2. Barabara itapitika kwa urahisi wakati wote
3. Barabara imeondoa vumbi kwa watumiaji
4. Barabara ya lami imeboresha usafiri, usafirishaji na mandhari ya Mji.


MRADI WA UKARABATI KITUO CHA AFYA NEMBA


Mradi huu wa ukarabati na Ujenzi wa Kituo cha Afya Nemba ulianza tarehe 01/09/2018 baada ya Halmashauri kupokea fedha kutoka Serikali Kuu kupitia programu ya uboreshaji wa Miundombinu ya kutolea huduma za Afya. Kiasi cha fedha kilichopokelewa ni Tsh.400,000,000/= kwa ajili ya Ukarabati na Ujenzi wa miundombinu katika Kituo cha Afya Nemba.
 LENGO LA MRADI
Ni kusaidia wananchi wapatao 20,189  kupata huduma za Afya kwa karibu na kwa urahisi zaidi, Kuondoa au kupunguza vifo vya Mama Wajawazito na watoto chini ya miaka mitano, Kupunguza vifo visivyo vya lazima pale mgonjwa anaposhindwa kwenda umbali mrefu kufuata huduma za Afya na Kuinua kiwango cha uchumi na uzalishaji kwa wananchi.


 VIPENGELE VYA MRADI
Mradi huu unahusisha ujenzi wa majengo yafuatayo:
i. Ujenzi wa Nyumba ya Mganga
ii. Ujenzi wa Maabara
iii. Ujenzi wa Wodi ya Watoto
iv. Ujenzi wa Nyumba ya kuhifadhi maiti
v. Ujenzi wa Wodi ya Wazazi na Jengo la Upasuaji

 GHARAMA ZA MRADI
Mradi huu umegharimu kiasi cha Tsh.411,400,000/= ambapo kiasi cha Tshs. 400,000,000/= ni fedha kutoka Serikali Kuu na Tshs. 11,400,000/= ni Mchango wa Jamii katika kusafisha eneo, uchimbaji wa Msingi na ujazaji wa kifusi majengo yote yaliyojengwa.


MRADI WA UBORESHAJI MIUNDOMBINU YA MAJI KATIKA MJI WA BIHARAMULO


Kutokana na umuhimu wa maji kwa viumbe hai ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2019 unasema “Maji ni Haki ya kila mtu, Tutunze vyanzo vyake na Tukumbuke Kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa”
Mradi huu wa ujenzi wa miundombinu ya maji ulianza tarehe 26/06/2018 baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa BUWASA kupata kibali cha kusaini Mkataba wa  Tshs 374,508,400 na Kampuni ya Evax Construction LTD ya Wilayani Muleba. Mradi huu wa maji  una mtandao wenye urefu wa km 6.58 katika eneo la Ng’ambo.

LENGO KUU LA MRADI  
i. Kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji kwa kuweka bomba kubwa lenye kipenyo cha 150mm.
ii. Kufunga bomba la urefu wa km 3.65 kupeleka maji (raising main) kutoka eneo la Kagango hadi eneo la Ng’ambo kwenye tanki la kuhifadhia maji lenye mita za ujazo wa 130.
iii. Kupanua  miundombinu ya usambazaji maji kwa kujenga mtandao wa maji wenye mabomba yenye vipenyo tofauti.
iv. Kuongeza vituo viwili (2) vya kutoa huduma ya maji eneo la Ngámbo.

WALENGWA
Walengwa wa mradi huu ni wakazi wote wa eneo la Ng’ambo wapatao 6,511.

GHARAMA ZA MRADI.
Gharama za mradi huu hadi hatua hii umegharimu kiasi cha Tsh. 374,508,400/= kwa mchanganuo ufuatao,


MRADI WA UJENZI WA VYUMBA VIWILI VYA MADARASA NA BWENI KWA AJILI YA WANAFUNZI WA KITENGO CHA ELIMU MAALUM SHULE YA MSINGI KABINDI  


Kitengo hiki cha Elimu Maalumu kilianzishwa hapa shuleni mwaka 2014 na kinaendelea kujengeka na kuimarika mwaka hadi mwaka. Hivi sasa kitengo kina wanafunzi 78 ikiwa wavulana 38 na wasichana 40,  ambao wapo katika makundi matatu ambayo ni  Walemavu wa akili 20 (Wavulana 10 na wasichana 10), Wasiosikia 54 (Wavulana 28 na Wasichana 26), wenye uoni hafifu 2 (Mvulana 1 na Msichana 1) na wenye usonji 2 (Mvulana 1 na Msichana 1).Mradi huu wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na bweni ulianza tarehe 03.09.2018 baada ya Halmashauri kupokea fedha kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).  

LENGO LA MRADI
Kuboresha mazingira kwa wanafunzi 80 wasichana kulala katika bweni na wanafunzi 50 kusoma katika vyumba viwili vya madarasa. Aidha wanafunzi 28 wataendelea kusoma katika chumba cha darasa kimoja (1) cha zamani.

GHARAMA ZA MRADI
Ndugu, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru,
Halmashauri imepokea Kiasi cha Tshs.Tsh.113,217,300/= kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa mchanganuo ufuatao:-
i.Kiasi cha Tsh. 75,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa bweni moja lenye uwezo wa kuchukua Wanafunzi 80 wa kike.
ii.Kiasi cha Tsh. 38,217,300/= kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO May 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHAJI VIFAA BAYOMETRIKI July 18, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • Tangazo la utoaji wa Mikopo ya Halmasahauri October 08, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • Mkurugenzi wa Uchaguzi Ndugu Ramadhani Kailima amewataka Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Tanzania bara kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

    June 16, 2024
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI SEHEMU YA PILI YA MPANGO HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO

    January 03, 2024
  • Waajiriwa wapya Division ya Afya na Elimu Juni, 2023

    June 07, 2023
  • MKUU WA MKOA WA KAGERA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI BIHARAMULO

    November 30, 2022
  • Tazama zaidi

Video

MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWAKA 2022 WILAYANI BIHARAMULO
Video Zaidi

Kuarasa za Haraka

  • Historia

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Tovuti ya Manispaa ya Bukoba
  • Tovuti ya wilaya ya Muleba
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Kuwasiliana nasi

    Mtaa wa Bomani

    Sanduku la Barua: S.L.P 70

    Telephone: 028 2223403

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@biharamulodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya Biharamulo. Haki zote zimehifadhiwa