• Malalamiko |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Wafanyakazi |
Biharamulo District Council Website
Biharamulo District Council Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Misingi
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uasfi na Mazingira
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Furusa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
    • Kamati za Kudumu
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Ofisi

HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO YAGAWA VITAMBULISHO VYA WAJASILIAMALI 83

Posted on: May 5th, 2021

Afisa Biashara wa Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera, Bahati  Dominick amesema vitambulisho vya  wajasiliamali wadogo vimetolewa kwa  wachache waliohakikiwa  ambao hawajahakikiwa ni wengi na wako vijiji  hivyo kuwataka watendaji wa kata na vijiji  kuwahamasisha wananchi juu ya umuhimu wa   kuwa na vitambulisho vya  wajasiliamali wadogo wadodo ili kufanya  biashara zao katika maeneo mbalimbali bila usumbufu.

Dominick ameyasema hayo wakati akitoa  taarifa  kwa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo  Kanali Mathias  Kahabi ,ambaye amewakilishwa na Mwenyekiti wa Halmashuri ya  Biharamulo Leo Rushahu  kwenye hafla  ya uzinduzi wa  vitambulisho vya wajasiliamali ambayo imefanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo  May 4, 2021.

Amesema mwaka 2019 walipokea vitambulisho 7770 na kuviuza ambapo mwaka 2020 walipokea vitambulisho 8600 kati ya hivyo vilivyouzwa 5774 na mwaka huu 2021 wamepokea vitambulisho 8200 ambavyo vimeuzwa ni vitambulisho 203 ila walivyo vikabidhi leo ni 83 ambavyo vimehakikiwa.

“Wajasiliamali ambao hawatahusika na kugawiwa vitambulisho nipamoja na mafundi welding, wanahusika na uchomeleaji wa vyuma, saluni kubwa, na wale wafanya biashara wakubwa wenye leseni”, Amesisitiza Dominick.

Dominick ameogeza kuwa kutakuwa na msako wa kukagua wajasiliamali wenye vitambulisho kabla hawajaingia sokoni, kwa wale ambao watakutwa hawana hawataruhusiwa kuingia sokoni hii itawasaidia kuepusha mgogoro kwa wale waliolipia.

Mwenyekiti  wa Halmashauri  ya Biharamulo, Leo Lushahu aliyemwakilisha  Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo  Kanali  Matias Kahabi  amesema  wajasiliamali wakilipia vitambulisho vya Tsh 20,000 elfu watapa haueni ya kulipa Tsh 1,000 elfu kila wanapo ingia sokoni ambapo kwa mwaka itakuwa zaidi laki moja.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo Dr Sospiter Mashamba,  amewaomba wajasiliamali kuwa mabarozi wazuri kwa wengine ili nao waweze kunufaika na vitambulisho   vilivyoboreshwa.

Akizungumza kwa niaba  ya Madiwani wa Halmashauri  ,Diwani wa Kata ya Biharamulo Mjini  Devidi  Mwenenkundwa   amewaomba viongozi watakaohusika na zoezi la kukagua  vitambulisho kutowasumbua wajasiliamali ambao wanakamilisha taratibu za kupata vitambulisho  hivyo.

Nae mjasiliamali wa Soko la Kasusula Biharamulo Mjini, Levina Jeremiah, amesema anaishukuru  sana Serikali kwa kuleta vitambulisho vya wajasiliamali maana vimekuwa neema kubwa kwao kwa kufanya biashara kwa uhuru bila kusumbuliwa.

Imeandikwa na  Kitengo cha Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 30, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 30, 2021
  • UKUSANYAJI WA MAPATO YA HALMASHAURI YA WILAYA BIHARAMULO January 14, 2019
  • TANGAZO LA NAFASI WAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA July 10, 2019
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • Matokeo ya mashindano ya Uandishi wa Insha kwa Shule za Msingi na Sekondari juu ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara na miaka 59 ya Jamhuri, Wilaya ya Biharamulo.

    December 17, 2021
  • STENDI YA MABASI KATA YA KABINDI WILAYA YA BIHARAMULO YAZINDULIWA

    June 04, 2021
  • MKUU WA WILAYA YA BIHARAMULO AWAHAKIKISHIA WANANCHI WAKE ULINZI NA USALAMA KWA KIPINDI HIKI CHA SIKUKUU YA EID EL FITRI

    May 12, 2021
  • MKUU WA WILAYA YA BIHARAMULO AIPONGEZA MENEGIMENTI YA HALMASHAURI HIYO KWA USIMAMIZI MZURI WA UJENZI WA HOSPITALI

    May 07, 2021
  • Tazama zaidi

Video

UZINDUZI WA HIFADHI YA TAIFA BURIGI
Video Zaidi

Kuarasa za Haraka

  • Historia

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Tovuti ya Manispaa ya Bukoba
  • Tovuti ya wilaya ya Muleba
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Kuwasiliana nasi

    Mtaa wa Bomani

    Sanduku la Barua: S.L.P 70

    Telephone: 028 2223403

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@biharamulodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya Biharamulo. Haki zote zimehifadhiwa