• Malalamiko |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Wafanyakazi |
Biharamulo District Council Website
Biharamulo District Council Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Misingi
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Miundombinu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uasfi na Mazingira
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Furusa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba ya Vikao
    • Kamati za Kudumu
  • Miradi
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mapato na Matumizi Robo ya Tatu
    • Jarida la eGA Toleo 6 na 9
    • Bajeti ya Mwaka 2023-2024
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Mkutano wa Baraza la Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Ofisi

STENDI YA MABASI KATA YA KABINDI WILAYA YA BIHARAMULO YAZINDULIWA

Posted on: June 4th, 2021

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera, Leo Lushahu awaomba wananchi wa kata ya Kabindi wasiogope kuwekeza katika stendi hiyo ili kuweza kukuza uchumi wa mji huo pia amewahakikishia ulinzi na usalama wa mali zao .

Ameyasema hayo baada ya uzinduzi wa stendi  mpya ya mabasi katika kijiji cha Kikomakoma kata ya Kabindi June, 4, 2021.

Lushahu, awasihi Vijana wa bodaboda kuchangamkia fursa ya kujiali katika stendi hiyo mpya kwa kuzingatia kanuni na taratibu zilizowekwa na sheria ya usalama barabarani.

“Tumejipanga kuhakikisha tunaboresha stendi hii kwa kiwango cha juu zaidi kutokana na ushirikiano wenu katika uwekezaji”, amesisitiza Lushahu.

Afisa Biashara wa Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera, Bahati Dominick amesema wanakusudia kuingiza magari takribani 150 kwa siku kwa ajili ya usafiri. Stendi hii ni mojawapo ya chanzo cha mapato ya Halmashauri ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi wa Halmashauri.

Dominick amesema kutakuwa na utaratibu wa kutoza ushuru kwa kila gari linalo ingia stendi kwa ajili ya kusafirisha abiria kama sehem zingine kwa gharama zifutazo Basi kubwa Tshs 3000 Tax Tshs 1000 Mini Bas Tshs 2000 na Costa Tshs 3000 Tunatarajia kukusanya mapato kupitia stendi hiyo kwa mwaka zaidi ya Tshs milioni 54,000,000.

Vilevile ameongezea kwamba wanatalajia kuanza kukusanya mapato ya Halmashauri 7/6/2021 pia anawaomba wananchi waweze kutoa ushirikiano ili waweze kuongeza mapato ya Halmashauri.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Biharamulo mjini Devidi Mwenenkundwa amewaomba wananchi wa kata ya kabindi kuiunga serikali mkono kwa ajiri ya kuinua uchumi wa Halmashauri pia kuwataka waache siasa wafanye kazi ya kimaendeleo katika stendi hiyo.

Afisa usalama barabarani kata ya Kabindi Magoma Peter, amewahakikishi wananchi wa kata ya Kabindi kwamba wamejipanga vizuri kuhakikisha wanazuia ajari katika eneo la stendi na atakae bainika anavunja sheria ya usalama barabarani hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Nae, Mwenyekiti wa wawekezaji Kikomakoma kata ya Kabindi Goderiva Binamungu amesema wawekezaji walifanikiwa kujenga vibanda kwa muitikio mkubwa ambapo vibanda 80 vimejengwa, kulipia kwa 100% eneo la wawekezaji, ushirikiano wa wawekezaji na afisa mtendaji wa kijiji.

Hatahivyo amezitaja changamoto mbalimbali zinazowakwamisha katika shughuli zao uhaba wa fedha za kumalizia ujenzi, wizi wa mali za wawekezaji mfano kuibiwa fremu za milango, mtazamo hasi wa jamii juu ya mradi wa soko na stendi.

Binamungu, ameyasema matarajio ya mradi wa stendi hiyo ni kuongeze kipato kwa wawekezaji, jamii na Serikali, kuongeze ajira kwa bodaboda , wajasiriamali wadogowadogo na kukua kwa mji, pia tunaiomba serikali kuimalisha ulinzi na usalama katika mali za wawekezaji katika eneo la stendi.

Imeandalikwa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo

Matangazo

  • TANGAZO KUHUSU UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA August 30, 2024
  • TANGAZO LA KUSHIRIKI UCHACUZI WA SERIKALI ZA MITAA November 23, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHAJI VIFAA BAYOMETRIKI July 18, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • Mkurugenzi wa Uchaguzi Ndugu Ramadhani Kailima amewataka Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Tanzania bara kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

    June 16, 2024
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI SEHEMU YA PILI YA MPANGO HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO

    January 03, 2024
  • Waajiriwa wapya Division ya Afya na Elimu Juni, 2023

    June 07, 2023
  • MKUU WA MKOA WA KAGERA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI BIHARAMULO

    November 30, 2022
  • Tazama zaidi

Video

MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWAKA 2022 WILAYANI BIHARAMULO
Video Zaidi

Kuarasa za Haraka

  • Historia

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Tovuti ya Manispaa ya Bukoba
  • Tovuti ya wilaya ya Muleba
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Kuwasiliana nasi

    Mtaa wa Bomani

    Sanduku la Barua: S.L.P 70

    Telephone: 028 2223403

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@biharamulodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya Biharamulo. Haki zote zimehifadhiwa